Psalms 20:1-4

Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)


1 a Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki,
jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.

2 bNa akutumie msaada kutoka patakatifu
na akupatie msaada kutoka Sayuni.

3 cNa azikumbuke dhabihu zako zote,
na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.

4 dNa akujalie haja ya moyo wako,
na aifanikishe mipango yako yote.
Copyright information for SwhKC